Friday, December 26, 2014

KATIBA YA ARITASO


WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI

CHUO CHA ARDHI TABORA
ARDHI INSTITUTE TABORA (ARITA)

  KATIBA 
YA 
JUMUIYA YA WANACHUO WA CHUO CHA
ARDHI TABORA
(Ardhi Institute Tabora Students’ Organization: (ARITASO)

                                                                      21 Octoba  2013

 
UTANGULIZI
Katiba hii ni matokeo ya maoni ya wanachuo wa Chuo cha Ardhi Tabora na imeandaliwa na Baraza la Wawakilishi la ARITASO kwa kuzingatia kifungu cha ibara 8.8 (l) cha katiba ya ARITASO ya mwaka 2006.

                                                               SHUKRANI
Shukrani  ziwaendee  wote  waliochangia  maoni  yao  kwa  ajiri  ya  kukamilisha  mchakato mzima  wa  Katiba  hii  ya  JUMUIA  YA  WANACHUO  CHUO  CHA  ARDHI  TABORA. Pia Tume inapenda  kuwashukru watu  wafuatao;
                          (i)Mkuu  wa chuo
                          (ii)Mwanasheria mkuu wa mkoani Tabora.
                          (iii)Wakufunzi wote wa chuo.
                          (iv)Wafanyakazi wote wa chuo
                          (v)Serikali ya wanachuo
                          (vi)Baraza la wawakilishi la Aritaso.
                          (vi)Taasisi mbalimbali.
                          (vii)Mlezi wa wanachuo
                          (viii)Wanachuo wote.
                          (ix)Wataalamu mbalimbali wa masuala ya katiba na watu binafsi.

  Imechapishwa:                                                                       Matendo   E.  Kabitagi.
                                                                                    Waziri  wa Sheria na  Katiba  ARITASO 
  21 Octoba 2013



MKUU  WA  CHUO
………………………….




Tamko

Sisi Wanachuo wa Chuo cha Ardhi Tabora tunaelewa na kuamini kuwa;

Chuo hiki kina umuhimu wa pekee katika maendeleo ya nchi yetu.

Na kwamba
Umoja wa Wanachuo ulio adilifu na wa kidemokrasia ndiyo utakaoweza kusimamia maslahi ya Wanachuo kikamilifu.

Hivyo basi sisi Wanachuo wa Chuo cha Ardhi Tabora tunatamka rasmi kuwa;
Kutakuwa na Umoja wa Wanachuo wa Chuo cha Ardhi Tabora utakaojulikana kwa jina la:
UMOJA WA WANACHUO WA CHUO CHA ARDHI TABORA
au
ARDHI INSTITUTE TABORA STUDENTS’ ORGANIZATION (ARITASO)

Ambao utakuwa na Madaraka yote ya Kikatiba kulingana na kanuni na Sheria za Chuo kama Ifuatavyo:

IBARA YA KWANZA

JINA, MAKAO MAKUU, KAULI MBIU, ANUANI NA LUGHA RASMI YA ARITASO

1.1 Jina la umoja wa Wanachuo wa Chuo cha Ardhi Tabora litakuwa:
UMOJA WA WANACHUO CHUO CHA ARDHI TABORA (ARITASO)
1.2  Makao Makuu ya ARITASO yatakuwa katika Chuo cha Ardhi Tabora.
1.3  Kauli mbiu ya Chuo ni “TAALUMA BORA YA ARDHI, MAENDELEO KWA TAIFA”
1.4  Anuani ya Chuo ni:-
             CHUO CHA ARDHI TABORA,
                S.L.P. 744, TABORA.

             SIMU: 026-260-4591.
                   FAX: 026-260-4928.
              Email: arita744@yahoo.co.uk
              E-mail ya ARITASO; aritaso@arita.ac.tz
                                           aritasoarita@gmail.com
              Blogu ya ARITASO: aritasoblog.blogspot.com

    Lugha rasmi;  

Itakuwa ni Kiswahili na Kiingereza

IBARA YA PILI

UFAFANUZI WA MANENO NA VIFUPISHO

Katika katiba hii ila iwapo maelezo yanayohitaji vinginevyo:-
Chuo cha Ardhi Tabora: Maana yake ni majengo, samani na jumuiya ya watu wote wanaoishi katika Chuo cha Ardhi Tabora.
2.1  Mwanachuo: Maana yake ni mtu yeyote anayesoma katika Chuo cha Ardhi Tabora.
2.2  Umoja wa wanachuo: Maana yake ni Umoja wa Wanachuo wote wanasoma chuo cha Ardhi Tabora chini ya ARDHI INSTITUTE TABORA STUDENTS’ ORGANIZATION (ARITASO)
2.3  Chuo: Maana yake ni Chuo cha Ardhi Tabora.
2.4  Baraza la Uendeshaji: Maana yake ni Rais, Makamu wa Rais, Katibu Mkuu, Mawaziri na Manaibu Mawaziri wa Wizara zote za ARITASO.
2.5  Waziri: Maana yake ni kiongozi wa Wizara yoyote ya ARITASO.
2.6  Viongozi Wakuu: Maana yake ni viongozi wakuu wa ARITASO ambao ni:-
i)        Mwenyekiti
ii)      Makamu Mwenyekiti
iii)    Katibu mkuu

2.7  Baraza la Wawakilishi: Maana yake ni Wawakilishi wote wa Wanachuo wa Chuo cha Ardhi Tabora ambao ni viongozi wote wa Aritaso ,Viongozi wa Mabweni na Wawakilishi wa madarasa
2.8  Spika: Maana yake kiongozi mkuu wa Baraza la wawakilishi na ndiye anayepaswa kuongoza vikao vyote vya Baraza la wawakilishi.
2.9  Naibu Spika: Maana yake ni Makamu wa Spika wa Baraza la Wawakilishi.
2.10          Kamati ya Nidhamu:  Maana yake ni kamati ya ARITASO inayoshughulikia nidhamu na maadili ya wana –ARITASO.
2.11Tume ya Uchaguzi: Maana yake ni kamati maalumu inayoshughulikia masuala yote      ya chaguzi za ARITASO
2.12  Uchaguzi Mkuu: Maana yake uchaguzi wa Rais na Makamu wa Rais.

IBARA YA TATU

MADHUMUNI;

3. Madhumuni ya ARITASO yatakuwa kama ifuatavyo:-

a)   Kuwa chombo cha pekee cha kulinda maslahi ya Wanachuo kwa muda wote      wanapokuwa Chuoni.
b)   Kujenga moyo wa kuheshimiana kusaidiana na kupendana baina ya Wanachuo na Jumuiya nyingine.
c)   Kuweka mawasiliano sahihi na ya kindugu baina ya Wanachuo na Uongozi wa Chuo pamoja na kudumisha uhusiano mzuri kati ya Wanachuo na Walimu / Wakufunzi, Wafanyakazi na jumuiya yote ya Chuo cha Ardhi Tabora, ili kuhakikisha Wanachuo wanapatiwa Elimu bora na inayoendana na wakati.
d)  Kuhakikisha kwamba kila Mwanachuo anaelewa na anatekeleza kikamilifu wajibu wake wa kujielimisha kwa kadiri ya uwezo wake.
e)   Kuimarisha ari ya kusoma na kujenga mazingira bora ya usomaji.
f)    Kuendeleza ari ya kuheshimu Mamlaka na kujielimisha.
g)   Kudumisha na kuendeleza utamaduni wa Taifa letu na kujenga moyo wa kupenda utamaduni wa taifa letu ili Chuo kiwe mahali pa kuzalisha mabingwa wa fani mbalimbali.
h)   Kuanzisha na kudumisha uhusiano mwema na Wanachuo wa Vyuo vingine hapa nchini, Afrika na duniani kote.
i)     Kufanya kila jitihada ya kuhakikisha kuwa madhumuni yaliyoelezwa hapa yanatekelezwa ipasavyo.
j)     Kubuni, kuanzisha,kusimamia na kuboresha miradi ya kuwasaidia wana Aritaso waliopo na wajao kwa mtindo wa kupeana kijiti.

IBARA YA NNE

KAZI ZA ARITASO:  

4.0Majukumu ya ARITASO.

Kwa kushirikiana na Mshauri wa Wanachuo (Dean of Students) katika kutekeleza madhumuni yake yaliyotajwa katika ibara ya tatu ya katiba hii, ARITASO itatekeleza kazi zifuatazo.
a)         Kuandaa shughuli mbalimbali kwa ajili ya manufaa ya Wanachuo.
b)         Kuandaa midahalo, semina, warsha, mikutano na ziara za kielimu kwa kushirikiana na mamlaka ya Chuo ili kubadilishana uzoefu na kupanuana mawazo.
c)         Kuchapisha jarida, vitabu, gazeti n.k, kwa madhumuni ya kupashana habari.
d)        Kushiriki katika shughuli za kutafuta fedha kadiri umoja wa Wanachuo utakavyoona inafaa na kukubalika na mamlaka ya Chuo.
e)          Kuwaalika Viongozi mbalimbali kuja kuzungumza na Wanachuo baada ya kuwasiliana na mamlaka ya Chuo kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa, kijamii na kitamaduni.
f)          Kukuza mawasiliano na kuimarisha uhusiano kati ya jumuiya nyingine za wanachuo ambazo zina madhumuni yanayolingana na yale ya ARITASO.
g)         Kuanzisha kamati ya Sekretarieti au Tume kwa ajli ya kuboresha utekelezaji wa madhumuni ya umoja huu.
h)         Kuimarisha shughuli yoyote ambayo inahusiana na madhumuni ya katiba hii.
i)            Kumfariji kwa hali na mali  mwanachuo yeyote anayepatwa na matatizo kama
      vile kufiwa,  kuugua au kupatwa na ajali.
j)           Kuwawakilisha wanachuo kwenye  vyombo  vya Chuo vya maamuzi na katika   
       vyombo vingine vya maamuzi ndani na nje ya Chuo kadri itakavyohitajika.
k)   Kuandaa hatua madhubuti za kushughulikia malalamiko ya wanachuo na    
      kuyapatia ufumbuzi kwa kushirikiana na Uongozi  wa Chuo.

IBARA YA TANO

KANUNI, TARATIBU NA MAMLAKA YA ARITASO

5.1 Kanuni na Taratibu za ARITASO

Katika utendaji kazi wake, ARITASO itatii sheria zote za Jamhuri ya muungano wa Tanzania. ARITASO itafuata sheria, kanuni na taratibu za Chuo cha Ardhi Tabora. Pamoja na hayo itaongozwa na kanuni zifuatazo;-
a)Uwazi na ukweli katika mambo  yake yote
b)      Uwajibikaji katika kanuni na matendo yake
c)Kutathmini uwajibikaji wake ili kuboresha utendaji kazi
d)     Kuzingatia maadili yanayokubalika katika jamii
e)ARITASO itaheshimu na kuzingatia haki sawa kwa wanachuo wote bila kujali tofauti zao za jinsi, dini, imani, rangi, kabila, ulemavu, umri, ndoa, taifa au utofauti wa kozi.

5.2 Mamlaka

      ARITASO kwa kushirikiana na Mshauri wa wanachuo (Dean of Students)  
      Itakuwa   Mamlaka ifuatayo:
a)      Kuandaa katiba ya ARITASO
b)      Kuandaa kanuni na taratibu za Uchaguzi na kuendesha chaguzi zote za ARITASO
c)      Kuandaa mikakati , sera na miongozo mizuri ya kujenga ARITASO
d)     Kuandaa kanuni na taratibu  nzuri za uendeshaji wa miradi na  matumizi ya fedha ya ARITASO
e)      Kuandaa kanuni na taratibu za utoaji wa huduma kwa wana-ARITASO.
f)       Kushirikiana na kutekeleza mipango mbalimbali hapa chuoni kadri itakavyoona inafaa.
g)      Kumchukulia hatua za kinidhamu mwanachuo yeyote atakaye vunja sheria, kanuni na taratibu za Chuo au/na katiba ya ARITASO kupitia Kamati yake ya Nidhamu kwa mujibu wa kanuni na sheria za Chuo.

IBARA YA SITA

UANACHAMA:

6.1 Kujiunga na Muungano wa wanachuo;-

      Mtu yeyote ambaye amesajiliwa kusoma katika Chuo cha Ardhi Tabora    
      atakuwa Mwanachama wa ARITASO  moja kwa moja hadi atakapomaliza mafunzo yake      
      endapo hatafukuzwa Chuo au kusitishiwa masomo yake.

 6.2 Vigezo na Masharti ya uanachama wa ARITASO

a)         Mwanachama wa ARITASO atatakiwa kulipa ada ya uanachama kiasi cha Tsh. 10,000/= kwa mwaka mara afikapo hapa Chuoni. Kiwango hiki kinaweza kubadilika kulingana na kupanda kwa gharama za maisha, pia hakirudishwi. Baraza la wawakilishi litapitisha mabadiliko hayo.
b)         Mwanachama atafaidika au kunufaika na mradi wa Aritaso pale atakapotoa matunda mazuri na pia kuchangia uboreshwaji wa miradi utakapopata hasara au kuhujumiwa.
c)         Mwanachama anatakiwa kuwa mwajibikaji katika shughuli zote za ARITASO.                                                                     

6.3 Kusitishwa uanachama.

      Mwanachama wa ARITASO atahesabiwa kwamba sio mwanachama wa ARITASO     
      endapo hatakuwa mwanachuo wa Chuo cha Ardhi Tabora kwa sababu yoyote ile.

IBARA YA SABA

HAKI ZA MWANACHAMA

7.1 Mwanachama wa ARITASO atakuwa na Haki zifuatazo:-

a.    Kushiriki katika shughuli zote zinazoandaliwa na ARITASO pamoja na mamlaka ya Chuo.

b.    Kuchagua, kuchaguliwa, au kuteuliwa katika nafasi yoyote ya Uongozi wa ARITASO.
c.    Kuangalia/kuona nyaraka za fedha na nyaraka zingine za ARITASO ambazo ni za bayana baada ya kuomba idhini ya kufanya hivyo kutoka kwa Katibu Mkuu wa ARITASO.

d.    Kujitetea na kutoa maelezo yake mbele ya kikao chochote cha ARITASO pamoja na kukata rufaa katika vikao vya juu yake na kwa kushirikiana na mamlaka ya Chuo.

e.    Kukosoa, pia kukosolewa katika vikao mbalimbali vya ARITASO.

f.    Kutoa mchango wa maoni yake waziwazi na bila woga katika vikao na mikutano inayomhusu kwa manufaa ya ARITASO na jumuiya nzima ya Chuo cha Ardhi Tabora.
g.   Kupatiwa matibabu kikamilifu kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na mamlaka ya Chuo.

IBARA YA NANE

WAJIBU WA MWANACHAMA

 8.1 Mwanachama wa ARITASO atakuwa na wajibu ufuatao;-

i)           Kuilinda na kuitii Katiba hii ya ARITASO.
ii)         Kujielimisha na kujiendeleza kwa kadiri ya uwezo wake na kutumia Elimu yake kwa faida ya Taifa. Kulipa michango mbalimbali ya kikatiba au michango mingineyo Kama itakavyoamuliwa na ARITASO kwa nyakati mbalinbali.
iii)       Kuhudhuria kikamilifu vipindi vya masomo, mikutano, maandamano halali, na kukamilisha shughuli zote za kitaaluma anazowajibika nazo kwa wakati kila siku. Kama vile taaluma, michezo na usafi ambapo ni kwa maeneo husika tu. Kwa mfano;- madarasani, mabwenini na maeneo yote yanayozunguka madarasa na mabweni.
iv)       Kutekeleza misingi ya nidhamu, kushiriki vema katika shughuli za Chuo.
v)         Kutunza, kuthamini na kulinda mali ya Chuo na miradi yote ya chuo.
vi)       Kuendeleza tabia na moyo wa umoja na upendo kwa Wanachuo wenzake na kwa wanajumuiya wote wa Chuo cha Ardhi Tabora.
vii)     Kudumisha nidhamu bora na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kumletea aibu yeye mwenyewe, ARITASO au Chuo na Taifa kwa ujumla

IBARA YA TISA

VIKAO VYA ARITASO:

9.1 Vikao halali vya ARITASO vitakuwa kama ifuatavyo:-

a)      Mkutano wa Baraza la Uendeshaji.
b)      Vikao vya Kamati ya Nidhamu.
c)      Mkutano mkuu wa Wanachuo wote.
d)     Mkutano wa Baraza la Wawakilishi,
e)      Mkutano wa Wanachuo wote na Uongozi wa Chuo.

 9.2 Mkutano wa Baraza la Uendeshaji

a)      Mkutano wa Baraza la Uendeshaji utajumuisha wajumbe wote wa Baraza hilo na wajumbe wengine ambao litaona vema kuwaalika.
b)      Mkutano wa Baraza la Uendeshaji utakutana si chini ya mara mbili kwa kila muhula wa masomo.

9.3 Waziri Mkuu atatoa taarifa ya mkutano wa Baraza la Uendeshaji

a)      Baada ya kuombwa na Rais kufanya hivyo au
b)      Baada ya kupokea ombi la maandishi lililotiwa sahihi na theluthi moja ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi au robo ya Wanachuo wote.
c)      Katibu Mkuu atatoa taarifa ya Mkutano wa Baraza la Uendeshaji ndani ya siku tatu baada ya kutakiwa kufanya hivyo.
9.1  Rais wa ARITASO atakuwa ndiye Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu wa Serikali    ya       Wanachuo, kama hayupo Makamu wa Rais ataongoza Mkutano.
9.2   Kiwango cha wajumbe wa Mkutano wa Baraza la Uendeshaji
       Mkutano wa Baraza la Uendeshaji utatakiwa uwe na zaidi ya nusu ya wajumbe wote    
       wanaostahili kuhudhuria mkutano huo.

 9.4 Kazi za Mkutano wa  Baraza la Uendeshaji:-

  1. Kuzungumzia mambo yote yanayohusu maslahi ya Wanachuo.
  2. Kujadili na kutoa maamuzi juu ya mapendekezo yoyote ya vikao vya chini yake ikiwa ni pamoja na kukubali au kutokubali hoja kutoka Baraza la Wawakilishi ya kutokuwa na imani na Rais wa ARITASO bila kuathiri kipengele cha (11.2.0) cha katiba hii.
  3. Kupitisha taarifa mbalimbali zitakazotolewa na Baraza la Wawakilishi.
  4. Kujadili na kupitisha Katiba ya ARITASO itakayoandaliwa na Baraza la Wawakilishi.

    9.5 Mkutano Mkuu wa Wanachuo wote:-

a.       Mkutano mkuu wa Wanachuo wote utajumuisha Wanachuo wote wanaochukua mafunzo katika Chuo cha Ardhi Tabora.

b.      Mkutano mkuu wa Wanachuo wote utakutana si chini ya mara moja kwa muhula, ila Mkutano Maalum unaweza kuitishwa wakati wowote ili kujadili masuala muhimu ya dharura.

c.       Rais wa ARITASO ndiye atakuwa Mwenyekiti wa Mkutano mkuu wa Wanachuo wote, kama hayupo Makamu wa Rais ataongoza mkutano.

d.      Kiwango cha wajumbe wa Mkutano mkuu wa Wanachuo wote kitakuwa zaidi ya nusu ya wajumbe wote wanaostahili kuhudhuria Mkutano wa Wanachuo wote ama Mkutano maalum.

e.       Mkuu wa Chuo atakutana na Wanachuo  mara mbili kwa muhula au zaidi pale itakapoonekana kuna haja ya Wanachuo kuonana naye.

  9.6 Kazi za Mkutano mkuu wa Wanachuo wote.


a.       Kuchambua na kuzitolea maamuzi au ushauri taarifa zinazowasilishwa kwake na Baraza la Uendeshaji.

b.      Kujadili masuala mbalimbali yenye maslahi na maendeleo kwa Wanachuo na Chuo kwa ujumla

c.       Utawachagua Rais na Makamu wa Rais wa ARITASO inapofikia wakati wa uchaguzi.

IBARA YA KUMI

MIHIMILI YA ARITASO


10.1 Kutakuwa na Mihimili mikuu mitatu ya ARITASO, ambayo ni;

i)           Baraza la Uendeshaji (Serikali ya ARITASO inayochaguliwa  na wanachuo)
ii)    Baraza la Wawakilishi
iii)   Kamati ya Nidhamu

Kila Mhimili utajitegemea katika utendaji kazi wake.

10.2 BARAZA LA WAWAKILISHI

Kutakuwa na Baraza la Wawakilishi la ARITASO   ambalo litakuwa na    
Wajumbe wafuatao:-
a.       Spika wa Baraza la Wawakilishi
b.      Naibu Spika
c.       Katibu Mkuu wa Baraza la Wawakilishi
d.      Baraza la Uendeshaji
e.       Wenyeviti wa Mabweni
f.       Makatibu wa Mabweni
g.      Mwakilishi mmoja toka kila darasa

10.3 Mikutano ya Baraza la Wawakilishi.

a)      Baraza la Wawakilishi litakutana si chini ya mara tatu kwa muhula.
b)      Spika ataongoza mikutano yote ya Baraza la Wawakilishi, kama hayupo Naibu Spika atashika nafasi hiyo, na kama wote wawili hawapo kikao kitamchagua Mwenyekiti wa muda.
c)      Spika atatakiwa kutoa tangazo la kikao hicho kwa umma na barua ya mwaliko kwa wajumbe wote wa kikao hicho cha Baraza la wawakilishi siku mbili kabla. Akishindwa kufanya hivyo moja kwa moja atatakiwa kujiudhuru kwenye nafasi yake na Naibu spika atashikilia nafasi yake.
d)     Endapo kuna jambo la dharura, Spika atakuwa na uwezo wa kuitisha kikao cha dharura cha baraza la wawakilishi endapo tu asilimia ishirini na tano (25%) ya wajumbe wa kikao hicho wamesaini kukubali kuitishwa kwa kikao hicho. Tangazo la muda mfupi zaidi(chini ya siku mbili) atalitoa bila kufungwa na kipengele cha 10.3 (c)

  10.4 Muda wa uongozi.

a.       Wajumbe wote wa Baraza la Wawakilishi wataongoza katika nafasi zao kwa muda wa mwaka mmoja. Wanaweza kuendelea katika awamu nyingine ya uongozi endapo watachaguliwa au kuteuliwa tena.
b.      Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi atasitishwa uanachama wake kwenye Baraza hilo, ikiwa atabainika na yafuatayo;
    i) Kutohudhuria vikao viwili vya Baraza la wawakilishi bila taarifa yoyote   ya       Maandishi kwa Spika.
     ii)       Kifo, kusitisha masomo, kufukuzwa Chuo au kusitishiwa usajili wa Chuo.
iii)             Mjumbe yeyote wa Baraza la wawakilishi aliyechaguliwa na wanachuo katika eneo lake mfano kozi yake, bweni lake n.k atasitishwa kuwa mjumbe wa Baraza  la wawakilishi endapo Spika atapokea waraka kutoka kwenye eneo hilo  uliosainiwa na wajumbe wasiopungua theruthi mbili ya watu  wote wanaokaa   eneo hilo unaotaka aondolewe kwenye nafasi yake ya kuwa mjumbe wa Baraza  la wawakilishi.
iv)             Kuondolewa katika nafasi yake anayoiwakilisha kwenye Baraza la           Wawakilishi   kutoka kwenye eneo analoliwakilisha.

 10.5 Malipo ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.

a.          Wajumbe wote wa Baraza la wawakilishi hawatalipwa mshahara wowote isipokuwa     tu watawezeshwa kifedha ili kufanikisha kutekeleza majukumu yao.
b.         Asilimia ishirini (20%) ya mapato yote ya  mwaka ya ARITASO itatumika      
 Kuwawezesha kifedha viongozi katika utaratibu ufuatao:-
  i)   Baraza la Uendeshaji - Asilimia arobaini na tano (45%) ya hiyo asilimia ishirini
 ii) Baraza la Wawakilishi – Asilimia ishirini na tano (25%) ya hiyo asilimia                        ishirini
iii)       Kamati ya nidhamu – Asilimia tisa (9%) ya hiyo asilimia ishirini
iv)       Tume ya Uchaguzi – Asilimia ishirini na moja (21%) ya hiyo asilimia ishirini

NB: Uwezeshwaji huu utafanyika kwa mujibu wa kanuni na taratibu za ARITASO kwa kushirikiana na Mshauri wa wanachuo na kiwango hicho kinaweza kubadilika kutokana na  sababu mbalimbali. Baraza la Wawakilishi litahusika kufanya mabadiliko hayo kama litakavyoona inafaa.

 10.6 Kazi za Baraza la Wawakilishi

           Baraza la Wawakilishi litakuwa na kazi zifuatazo:-

a.       Kumchagua Spika, Naibu Spika na Katibu wa Baraza la wawakilishi.
b.      Kuthibitisha Mawaziri na Makatibu waliopendekezwa na Mwenyekiti kwa kushirikiana na Makamu wa Mwenyekiti na Katibu Mkuu wa ARITASO.

c.       Kuthibitisha Majina ya Wajumbe wasiopungua watano wa kuingia katika kila Wizara kama yatakavyopendekezwa na kamati ya Uendeshaji.

d.      Kuziangalia na kuzikubali au kuzikataa sera na mwenendo wa Baraza la Uendeshaji.

e.       Kupitisha makisio ya mapato na matumizi ya ARITASO kama yatakavyowasilishwa na Katibu Mkuu baada ya kutayarishwa na kamati ya Uendeshaji.

f.       Kuweka utaratibu wa uendeshaji wa mambo yote yanayohusu fedha za miradi ya ARITASO, ukaguzi wa mara kwa mara wa vitabu vya mahesabu na kutoa ripoti ya mwaka ya ukaguzi wa mahesabu yote.

g.      Kumteua mkaguzi wa ndani wa mahesabu ya ARITASO.

h.      Kufanya uchunguzi na kuchukua hatua za kinidhamu au za kisheria dhidi ya kiongozi yeyote wa ARITASO ama wengineo atakayebainika kuwa amehusika na matumizi mabaya ya fedha za ARITASO au ubadhirifu wa aina yoyote.

i.        Kumwondoa Madarakani Mwenyekiti au Makamu Mwenyekiti wa ARITASO  kwa kutumia utaratibu ulioainishwa kwenye ibara 11.2.0 ya katiba hii.

j.        Kuunda Idara na kamati za ARITASO kama zitakavyowasilishwa na kamati ya Uendeshaji kadiri itakavyoonekana ni lazima kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali.

k.      Kupokea Taarifa za Wizara na kamati za ARITASO.

l.        Kuandaa rasimu ya katiba ya ARITASO na kuipeleka mbele ya Mkutano Mkuu wa Wanachuo kwa kujadiliwa na kuthibitishwa kama ilivyoanishwa katika ibara ya 13. Ya katiba hii.

m.    Kufanya kazi zozote kama Mkutano Mkuu wa Serikali ya Wanachuo au/na Mkutano wa Wanachuo wote utakavyoagiza.

       10.7 Spika wa Baraza la wawakilishi.

i) Kutakuwa na Spika wa Baraza la wawakilishi atakaye chaguliwa kutoka                     miongoni wa wajumbe wa baraza hilo.
ii)   Spika hatakuwa mjumbe wa Baraza la Uendeshaji la ARITASO.
i)        Spika ataongoza vikao vyote vya Baraza la wawakilishi kwa mujibu wa  kanuni  na taratibu zote za Baraza hilo lililojiwekea.
ii)      Endapo Spika  atavunja kipengele chochote cha katiba hii,  Baraza la   
      Wawakilishi litakuwa na uwezo wa kumwondoa katika nafasi yake ya uspika kwa   
      Wajumbe wa Baraza hili kupiga kura zisizopungua theluthi mbili ya wajumbe       
      wote wa   baraza   hili.
v)      Spika atakuwa mwakilishi wa Baraza la Wawakilishi popote itakapohitajika     uwakilishi wa Baraza hili.

10.8 Naibu Spika

i)     Kutakuwa na Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi atakaye chaguliwa   kutoka miongoni mwa wajumbe wa baraza hili.
ii)   Naibu Spika hatakuwa mjumbe wa Baraza la Uendeshaji la ARITASO. Na atatakiwa kuongoza vikao vyote vya Baraza la Wawakilishi endapo Spika hayupo.
iii) Naibu Spika ataondolewa madarakani vilevile kama atakavyoondolewa Spika kama ilivyotamkwa kwanye ibara ya 10.7. (iv) ya katiba hii.

 10.9 Katibu wa Baraza la Wawakilishi.

i)        Kutakuwa na Katibu wa Baraza la Wawakilishi ambaye atachaguliwa na  wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutoka miongoni mwa wanachama wa   ARITASO.
ii)       Katibu wa Baraza la Wawakilishi atakuwa ndiye mwandishi na mtunza          nyaraka zote za Baraza la Wawakilishi. Pia atalazimika kufuata kanuni na   taratibu zote za baraza hili lillojiwekea.
iii)    Katibu wa Baraza la Wawakilishi anaweza kuondolewa madarakani kama                   Anavyoodolewa Spika wa Baraza hili kama ilivyotamkwa kwanye ibara ya                   10.7.(iv)    ya katiba hii.

10.10 BARAZA LA UENDESHAJI

i)        Kutakuwa na Baraza la Uendeshaji la ARITASO ambalo litakuwa ndicho chombo   cha kusimamia utekelezaji wa shughuli za kila siku za ARITASO. Baraza hili   litakuwa na Wajumbe wafuatao:-
a)      Rais wa ARITASO
b)      Makamu   wa Rais wa ARITASO
c)      Katibu Mkuu wa ARITASO
d)     Mawaziri wote wa Wizara za ARITASO
e)      Manaibu Mawaziri wote wa Wizara zote za ARITASO.
ii)   Baraza la Uendeshaji litakutana si chini ya mara tatu kila muhula.
iii)          Baraza la Uendeshaji litakuwa  na wajumbe wasiozidi  ishirini na moja ambao    watateuliwa kutoka miongoni mwa wanachama wa ARITASO.
iv)    Baraza la Uendeshaji litakuwa ndicho chombo kikuu cha kumshauri Rais juu ya  mambo yote yanayohusika na utekelezaji wa madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii, na  litamsaidia na kumshauri Rais juu ya jambo lolote litakalowasilishwa kwenye Baraza hilo kwa mujibu wa maagizo maalum au maagizo ya jumla yatakayotolewa na Rais.
v)      Rais wa ARITASO ataongoza vikao vyote vya Baraza la Uendeshaji.
vi)    Makamu wa Rais wa ARITASO atakaimu nafasi ya Rais kama Rais hayupo.
vii)  Mwenyekiti wa muda atateuliwa kuendesha kikao kama Rais na Makamu wa Rais hawapo.

10.11 Muda wa Uongozi.

a)   Mawaziri wote, manaibu waziri wote na makatibu wote wa wizara zote za ARITASO wataongoza katika nafasi zao kwa muda wa mwaka mmoja. Wanaweza kuendelea katika awamu nyingine ya uongozi endapo watachaguliwa au kuteuliwa tena.
b)   Waziri yeyote, naibu waziri yeyote au katibu  yeyote wa wizara  yoyote ya ARITASO atavuliwa nafasi yake ya uwaziri au unaibu waziri au ukatibu kwenye Baraza hilo, endapo atabainika na yafuatayo;

i)  Kutohudhuria vikao viwili vya Baraza la Uendeshaji bila taarifa yoyote   ya maandishi kwa katibu mkuu wa ARITASO
ii )  Kifo, kusitisha masomo, kufukuzwa Chuo au kusitishiwa usajili wa   Chuo.      
iii) Rais wa ARITASO   atakuwa na mamlaka ya kumwondoa Madarakani Waziri yeyote au naibu waziri yeyote kwa barua kwa utovu wa   nidhamu au kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake na atateua   mtu Mwingine kushikilia nafasi yake. Rais wa ARITASO atatoa taarifa  kwa barua kwenye Baraza la Wawakilishi juu ya uamuzi aliouchukua wa    kumwondoa madarakani kiongozi huyo.

10.12 Kazi za Baraza la Uendeshaji:-

a.    Kuongoza na kuendesha shughuli za kila siku za Wanachuo kwa mujibu wa Katiba hii na kama itakavyoagizwa na vikao vya juu vya ARITASO.
b.   Kusimamia maslahi ya kila siku ya Wanachuo.
c.    Kuidhinisha na kuthibitisha mapato na matumizi yote ya fedha za miradi ya Wanachuo.

d.   Kusimamia uzalishajimali na shughuli za uchumi za Wanachuo.
e.    Kusimamia utekelezaji wa Kanuni za Chuo na nidhamu ya Wanachuo kwa ujumla.
f.    Kupendekeza Wizara na kamati mbalimbali za ARITASO na kuwasilisha mbele ya
Baraza la Wawakilishi kwa uthibitisho, kwa mfano:-
                          i.   Wizara ya Chakula (Cafeteria)
                        ii.   Wizara ya Afya na Mazingira
                      iii.   Wizara ya Michezo, Habari na Mawasiliano
                      iv.   Wizara ya Elimu
                        v.   Wizara ya Sheria na Katiba
                      vi.   Wizara ya Mambo ya Ndani
                    vii.   Wizara ya Ulinzi na Usalama
                  viii.   Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano.

g.         Kuandaa makisio ya mapato na matumizi ya ARITASO  ya kila Wizara yatakavyowasilishwa na Waziri husika wa kila Wizara kwenye Baraza la wawakilishi.
h.         Kuandaa miswaada, kanuni, taratibu na sheria za ARITASO zitakazowasilishwa kwenye Baraza la wawakilishi ili kuidhinishwa.
i.           Ili kuondoa wasiwasi Mawaziri wote, manaibu  waziri wote na makatibu  wa Wizara  zote, wote watawajibika kwa  Rais wa ARITASO.

10.13 Malipo ya wajumbe wa Baraza la Uendeshaji

Ili kuondoa wasiwasi Wajumbe wote wa Baraza la wawakilishi hawatalipwa mshahara
wowote isipokuwa watawezeshwa kifedha ili kufanikisha utendaji kazi wao kama ilivyo tamkwa katika ibara ya 10.5 (b) ya katiba hii. 

10.14 KAMATI YA NIDHAMU

a)      Kutakuwa na Kamati ya nidhamu ya ARITASO ambayo itateuliwa na Raisi wa Aritaso mara baada ya kuingia madarakani. Kamati hii itakuwa na Mwenyekiti  na Katibu ambao ni waziri wa sheria na katiba pamoja na katibu kutoka ndani ya wajumbe wa kamati hiyo..
b)      Wajumbe wa kamati hii ni;-
i)        Mwenyekiti  wa kamati
ii)      Katibu wa kamati
iii)    Mjumbe  mmoja mmoja toka kila darasa.

10.15 Kazi za Kamati ya Nidhamu

i)     Ni chombo cha kudhibiti nidhamu ya wanachama wa ARITASO. Kamati hii itakuwa ndicho chombo   chenye mamlaka ya kutoa adhabu kwa ngazi ya wanachuo na kitatoa adhabu kwa   mwanachuo yeyote isipokuwa kwa Rais na Makamu wa Rais. Kamati hii itatoa adhabu kwa   makosa ya ubadhilifu wa mali ya ARITASO, rushwa na makosa mengine yote ya utovu wa nidhamu.
ii) Kuandaa kanuni na taratibu zote kwa ajili ya kupokea na kutatua migogoro miongoni   mwa wanachuo ili kuondoa matabaka ya ukozi rangi, jinsia n.k na ili   kuleta  haki, usawa, umoja na mshikamano miongoni mwa wanachuo.
iii) Kutekeleza maelekezo au majukumu yatakayotolewa na Baraza la wawakilishi, Baraza la  Uendeshaji au mwana ARITASO yeyote kama kuna hitajika kufanya   hivyo.

10.16 Mipaka ya utendaji wa kazi yake

a)         Kwa kushirikiana na mshauri wa wanachuo, kamati ya nidhamu ya Aritaso itakuwa ndicho chombo cha mwisho katika kutoa maamuzi ya migogoro chuoni ngazi ya wanachuo na yale yote yatakayoshindikana kupatiwa ufumbuzi katika kamati hii, kwa maandishi itayawasilisha kwenye ngazi ya Chuo ili kupatiwa ufumbuzi.
b)         Endapo kutahitajika, kamati hii inaweza kumwalika Rais wa ARITASO, Makamu wa Rais, Spika, kiongozi yeyote  au mtu yeyote ambaye kwa namna moja au nyingine kamati itamwitaji ili atoe mawazo yake, ushauri au/na ushahidi wa mambo mbalimbali yanayo hitaji msaada wake.

10.17 Muda wa uongozi

a)      Kamati hii itaongoza kwa muda wa mwaka mmoja tangu iingie madarakani.
b)      Mjumbe yeyote wa kamati hii atatakiwa kuondoka madarakani mara moja iwapo asipohudhuria vikao viwili vya kamati hii bila taarifa yoyote ya maandishi kwa Mwenyekiti wa kamati au kwa mtu yeyote anayekaimu nafasi hiyo.

10.18 Vikao vya Kamati ya Nidhamu

a)      Vikao vyote vya Kamati ya nidhamu vitaandaliwa na katibu wa kamati hii baada ya kushauriana na mwenyekiti wa kamati hii. Katibu atatakiwa kutoa tangazo la kikao hiki siku moja kabla ya siku ya kikao hicho.
b)      Wajumbe katika kikao hiki wanatakiwa wasipungue theluthi mbili ya wajumbe wote.
c)      Baraza hili litafanya vikao visivyopungua vitatu kila muhula wa  masomo.
d)     Endapo katibu wa Kamati hii atashindwa kuitisha kikao cha Kamati  au likitokea swala linalohitaji ulazima wa kuitisha kikao cha kamati, theluthi moja ya wajumbe wa kamati hii watakubaliana watamwomba katibu wa kamati  kuitisha kikao cha kamati hii ili kutatua swala lililojitokeza.

10.19 Malipo ya wajumbe wa Kamati ya Nidhamu

Ili kuondoa wasiwasi, Wajumbe wote wa Kamati ya Nidhamu hawatalipwa mshahara isipokuwa watawezeshwa kidogo kifedha ili kufanikisha utendaji kazi wao kama ilivyo tamkwa katika ibara ya 10.5 (b) ya katiba hii.  

IBARA YA KUMI NA MOJA

UONGOZI WA ARITASO NA KAZI ZAO.


11.1 Viongozi wa ARITASO watakuwa:-

a.       Rais i wa ARITASO
b.      Makamu wa Rais wa ARITASO
c.       Katibu Mkuu wa ARITASO
d.      Spika wa Baraza la wawakilishi
e.       Mawaziri wa Wizara zote za ARITASO
f.       Makatibu (ma-Naibu waziri) wa Wizara zote za ARITASO
g.      Wenyeviti wa Mabweni
h.      Makatibu wa Mabweni
i.        Wawakilishi wa Madarasa
j.        Wawakilishi Wasaidizi wa Madarasa

11.2    Rais wa ARITASO

a)         Rais wa ARITASO atachaguliwa na Mkutano Mkuu wa Wanachuo kwa kura za siri kwa mujibu wa katiba hii na kwa mujibu wa mwongozo na kanuni zitakazo kubaliwa na Baraza la wawakilishi.
b)         Rais wa ARITASO ndiye kiongozi Mkuu na Msemaji Mkuu wa ARITASO.
c)         Rais wa ARITASO atakuwa na uwezo wa kuteua Mawaziri wa Wizara mbalimbali kwa kushirikiana na Makamu wa Rais na Katibu Mkuu wa ARITASO.
d)        Uongozi wa ARITASO utasimikwa rasmi na Uongozi wa Chuo kama ilivyotamkwa kwenye ibara ya 12.  Ya katiba hii.
e)         Rais wa ARITASO ataongoza vikao vyote vya juu vya ARITASO, Wajumbe watamchagua Mwenyekiti wa muda iwapo Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti hawapo kama kifungu cha Katiba kinavyoagiza.
f)          Ikitokea Ofisi ya Rais wa ARITASO ikabaki wazi kabla ya nusu mwaka kuisha (nusu ya muda wake wa uongozi), uchaguzi utafanyika haraka ili kuziba pengo hilo au namna nyingine inaweza kufanyika kama itakavyoamuliwa na Baraza la wawakilishi ili kuziba pengo hilo na izingatiwe kwamba kama mwenyekiti amekaa madarakani kwa muda wa nusu mwaka (nusu ya muda wake wa uongozi) uchaguzi hautafanyika na badala yake makamu mwenyekiti atashikilia ofisi ya Mwenyekiti wa ARITASO ili kumalizia muda uliobaki.
g)         Sababu za kubaki  wazi kwa Ofisi ya Rais wa ARITASO ;-
i)     Kujiuzuru kwa kwa Rais wa ARITASO
ii)         Kifo
iii)       Kuondolewa madarakani.
iv)       Kusitishiwa masomo au kufukuzwa Chuo
v)         Sababu nyingine yoyote ile inayoweza kupelekea Ofisi ya Rais ARITASO kubaki wazi.
a)         Endapo Rais wa ARITASO hatakuwepo ofisini  kwa sababu yoyote ile kama vile kusafiri au dharura yoyoye ile, majukumu ya Ofisi ya Rais ARITASO atamwachia yeyote kati ya hawa  wafuatao kwa kufuata mpangilio;
i)  Makamu  wa Rais ARITASO
ii)  Waziri Mkuu
ii)  Spika

NB.Mtu  yeyote kati ya hao yaani kipengele 11.1.8 a),b),c) hapo juu aliye achiwa madaraka, atakabidhi madaraka hayo haraka iwezekanavyo, baada ya mtu aliyemkabidhi kurudi.

 11.3 Kuvunjika kwa Serikali

Kama nafasi ya Rais wa ARITASO na Makamu wa Rais imebaki wazi kwa sababu zozote zile kama katiba hii inavyotamka, Serikali nzima ya ARITASO itahesabika kuwa imevunjika. Katika hali hii Wajumbe wengine wa Baraza la Uendeshaji wataendelea kushikilia nafasi zao za uongozi hadi pale Uchaguzi Mkuu utakapo fanyika ili kumpata Rais na makamu wa Rais mpya. Uchaguzi huo utatakiwa ufanyike ndani ya siku kumi na nne baada ya nafasi hizo kubaki wazi.

 11.4 Vigezo vitakavyo tumika kumchagua Rais wa ARITASO.

a)            Mwanachama yeyote wa ARITASO ataruhusiwa kuchaguliwa kuwa Rais wa ARITASO ikiwa tu ana muda wa mwaka mmoja au zaidi wa uanachama wake ndani ya ARITASO.
b)            Mtu yeyote anayeshikilia wadhifa wa Rais wa ARITASO ataruhusiwa kugombea tena katika nafasi hiyo.
c)            Mtu aliyechaguliwa kuwa Rais wa ARITASO, asipo jiuzuru,au asipofariki au asipoondolewa madarakani au asipositishiwa masomo yake atashikilia Ofisi hiyo ya Rais wa ARITASO kwa muda usiopungua mwaka mmoja.

 11.5 Kumwondoa Rais wa ARITASO Madarakani

a)               Baraza la wawakilishi litakuwa na uwezo wa kupitisha maamuzi ya kumwondoa     
Rais wa ARITASO madarakani kama ilivyotamkwa katika kipengele cha 10.6.(i) cha katiba hii.
b) Sababu za kumwondoa Rais madarakani ni kama ifuatavyo;-
i) Akifanya vitendo viovu vinavyovunja katiba hii.
ii) Akifanya vitendo vinavyoishushia heshima ofisi ya Rais wa ARITASO.
c) Waraka wowote wa kumwondoa Rais madarakani lazima usainiwe na theluthi   
     mbili ya wajumbe wote wa Baraza la Wawakilishi na uambatanishwe na saini za   wanachuo kumi kutoka kila kozi na ziwasilishwe kwa Spika.
d)     Kabla ya Baraza la Wawakilishi kutoa maamuzi ya kumwondoa Rais madarakani,  yafuatayo yatazingatiwa;-
i)        Kwa idhini ya maadishi ya Spika, itaundwa kamati ya uchunguzi ya watu watano, na majina yao yataidhinishwa na theluthi mbili ya wajumbe wote    Baraza la Wawakilishi.
ii)      Kamati hii itafanya uchunguzi juu ya tuhuma kwa Rais na itatakiwa itoe taarifa yake ya uchunguzi kwa Spika ndani ya  siku saba toka siku   majina ya tume hiyo  yalipotangazwa.
iii)    Spika atatakiwa kumtaarifu Rais juu ya tuhuma zinazomwandama.iv) Spika atakapopokea ripoti ya kamati ya uchunguzi, atatakiwa kuitisha mkutano wa  dharura wa Baraza la Wawalishi ili ripoti ya kamati ya uchunguzi isomwe na mwenyekiti wa kamati hiyo mbele ya Baraza la wawakilishi. Kisha Baraza la wawakilishi litatathmini ripoti hiyo.
iv)    iv) Spika atampa barua Rais juu ya matokeo ya uchunguzi wa kamati ya uchunguzi pamoja na maamuzi ya Baraza la wawalishi. Rais atatakiwa kujitetea   juu ya    tuhuma hizo na atatakiwa kutoa taarifa yake ya kujitetea ndani ya siku tatu mbele ya Baraza la wawakilishi na/au atawasilisha taarifa yake  ya maandishi ya kujitetea kwa   Spika.
v)      Spika atatakiwa kuitisha Mkutano Maalum wa Baraza la wawakilishi  kwa ajili ya kutoa maamuzi ya kumwondoa  au kutomwondoa  Rais madarakani kwa kuzingatia ile ripoti ya kamati ya uchunguzi na taarifa ya kujitetea ya  Rais.Uamuzi wa kumwondoa Rais madarakani utafikiwa tu endapo theluthi mbili ya wajumbe wa Baraza la wawakilishi watakubali uamuzi huo.
vi)    Wajumbe wa Mkutano Maalum wa Baraza la wawakilishi wa kutoa uamuzi wa kumwondoa au kutomwondoa Rais madarakani wanatakiwa wasipungue asilimia tisini (90%) ya wajumbe wote wa baraza hilo.
vii)  Baraza la wawakilishi litakapopitisha uamuzi wa kumwondoa Rais madarakani kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na katiba hii, Rais atatakiwa kuondoka madarakani mara moja mara tu baada ya uamuzi huo kupitishwa na Baraza hilo na kwamba Serikali yote ya ARITASO itakuwa imevunjika. Makamu wa Rais na waziri mkuu wataendelea kubaki madarakani ilimradi wawe hawahusiki na tuhuma za Rais. Na utaratibu wa kipengele cha 11.2 (f) cha katiba hii utazingatiwa.

11.6   Makamu wa Rais wa ARITASO

a)  Makamu wa Rais wa ARITASO atachaguliwa na Mkutano Mkuu wa Wanachuo    
         kwa kura za siri kwa mujibu wa taratibu zitakazo wekwa na Baraza la    
         wawakilishi.
b) Makamu wa Rais wa ARITASO ni msaidizi mkuu wa Rais wa ARITASO.
c) Atakuwa ndiye Mwenyekiti wa mikutano yote iwapo Rais wa ARITASO hatakuwepo.
d) Atafanya kazi nyingine zote kwa kushauriana na Rais wa ARITASO.

11.7Katibu Mkuu wa ARITASO.

i) Rais wa ARITASO kwa kushirikiana na Makamu Rais wa ARITASO watamteua Katibu Mkuu wa ARITASO.
ii) Katibu Mkuu atakuwa ndiye mtendaji mkuu wa ARITASO.
iii) Atashughulikia maswala yote yanayohusu matatizo mbalimbali ya Wanachuo.
iv) Atakuwa mratibu wa shughuli zote za Wizara na za Kamati mbalimbali, ikiwa ni     pamoja na kuandaa taarifa zote za ARITASO.
v) Atakuwa mwandishi wa mihutasari yote ya mikutano yote ya ARITASO. Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, Waziri Mkuu atawajibika kwa Rais kuhusu utekelezaji wa madaraka yake.

 11.8 Mawaziri wa Wizara mbalimbali.

b)      Kutakuwa na Mawaziri mbalimbali wa ARITASO ambao watateuliwa na Rais kwa kushirikiana na Makamu  wa Rais na Katibu Mkuu wa ARITASO ambao watasimikwa na Uongozi wa Chuo kama ilivyotamkwa katika ibara ya 13. Ya katiba hii.
iii)    Mawaziri watakuwa ndio watendaji wakuu wa Wizara zao.
Mawaziri watafanya kazi zote chini ya Uongozi wa Rais, Makamu wa Rais na Katibu Mkuu.

11.9 Makatibu wa Wizara

i) Kutakuwa na Makatibu wa Wizara mbalimbali za ARITASO ambao ndio watakaokuwa Ma-Naibu Mawaziri wa Wizara husika.
iv) Makatibu watasimamia utekelezaji wa shughuli za kila siku za Wizara zao.

11.10  Wenyekiti wa Mabweni

a)      Kutakuwa na Wenyeviti wa Mabweni ya Wanachuo ambao watachaguliwa na wakazi wote wa Mabweni husika kwa kura za siri.
b)      Mwenyekiti wa bweni atakuwa ndiye Kiongozi Mkuu wa Bweni.
c)      Atakuwa ndiye Mwenyekiti wa vikao vyote vya bweni.

11.11 Makatibu wa mabweni

a)      Kutakuwa na ma-Katibu wa mabweni (ambao ndio Makamu wenyeviti) katika kila bweni ambao watachaguliwa na Wakazi wote wa bweni linalohusika kwa kura za siri.
b)      Katibu wa Bweni atakuwa ndiye mtendaji Mkuu wa Bweni.
c)      Katibu wa bweni atafanya kazi zake zote chini ya Baraza la  Uendeshaji.

11.12 Kazi za Makamu / Katibu wa Bweni.

i)        Atakuwa ndiye kiongozi Mkuu wa eneo la Bweni lake.  Kazi zake kusimamia ulinzi na usalama wa Bweni lake.
ii)      Kupanga na kusimamia kazi za usafi wa eneo lake.
iii)    Kusimamia nidhamu na mwenendo mwema wa wakazi wote wa eneo lake la    
        Bweni na kutoa Taarifa ya utovu wa nidhamu wa Mwanachuo yeyote kwa   
        Mwenyekiti wa Bweni au kwenye mamlaka ya juu.
iv)    Kuhakikisha kuwa wakazi wote wa eneo lake la ubalozi hawavuti sigara, hawapiki vyakula, kupiga pasi au kuchemsha maji kwa kutumia ‘heater’ katika vyumba vya kulala kwa ajili ya usalama wa majengo na Wanachuo wenyewe.
v)      Kutoa taarifa ya wizi au upotevu wa mali ya Chuo au ya Mwanachuo kwa Mwenyekiti wa bweni au kwa uongozi wa juu.
vi)    Kuhakikisha kuwa daima kuna hali ya utulivu, amani na ushirikiano mzuri  miongoni mwa wakazi wote wa bweni lake.  

11.13 Kamati ya Bweni

i.      Kutakuwa na Kamati ya Bweni katika kila Bweni ambayo itakuwa na wajumbe wafuatao:-
a)      Mwenyekiti wa Bweni
b)      Katibu wa Bweni (Makamu Mwenyekiti)
ii.   Mwenyekiti wa Bweni ataongoza mikutano yote ya Bweni na Katibu wa Bweni atakuwa ndiye mwandishi wa vikao vyote vya Bweni.
iii.   Idadi ya wajumbe katika mkutano wa bweni isipungue nusu ya wakazi wote wa bweni husika.
iv.                  Kamati ya bweni itakutana si chini ya mara moja kwa wiki mbili.

11.14 Kamati ya Bweni itakuwa na haki zifuatazo:-

a)   Kusimamia ulinzi na usalama wa bweni ikishirikiana na wajumbe wa Wizara ya Ulinzi na Usalama.
b)   Kusimamia na kuongoza kazi za kila siku za Bweni kwa maslahi ya wakazi wa   bweni.
c)   Kushughulikia matatizo ya jumla na ya binafsi ya wakazi wa Bweni, usafi wa bweni wa ndani na nje na kuhakikisha kuwa Bweni linakuwa na utulivu.
d)  Kutekeleza uamuzi wa mkutano wa Bweni na vikao vingine vya juu.

11.15 Wawakilishi wa Madarasa

a)   Kutakuwa na Wawakilishi wawili kwa kila darasa ambao watachaguliwa na wanachuo wa darasa linalohusika kwa kura za wazi. Viongozi hao watakuwa na kazi  zifuatazo:-
b)   Kusimamia nidhamu ya Darasa lake na kutoa taarifa ya utovu wa nidhamu wa  Mwanachuo yeyote kwa uongozi wa juu wa ARITASO.
c)  Kuweka kumbukumbu za mahudhurio ya Wanachuo wa darasa kwa kila kipindi na kila siku.

IBARA YA KUMI NA MBILI

UCHAGUZI NA UTEUZI WA VIONGOZI WA ARITASO

12.1 Tume ya Uchaguzi.

 a) Kutakuwa na Tume ya Uchaguzi ambayo itasimamia shughuli zote za Uchaguzi   wa   Viongozi wa ARITASO chini ya uangalizi na usimamizi wa kamati ya nidhamu.
b) Tume ya uchaguzi itateuliwa wiki nne baada ya kuanza kwa mwaka mpya wa  masomo.   
c) Mwenyekiti na makamu mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi watachaguliwa kutoka   miongoni mwa wajumbe wa Tume hiyo.
d) Tume ya Uchaguzi itakuwa na mamlaka kamili  ya kuendesha na kusimamia chaguzi za   
      ARITASO kwa mujibu wa taratibu na kanuni za uchaguzi za ARITASO.Tume hii  
      itakuwa   na mamlaka ya kutangaza matokeo ya chaguzi na ndiyo itakuwa yenye   
      maamuzi ya  mwisho kuhusu  masuala ya uchaguzi  zaidi ya hapo mwenye kulalamika   
      juu ya masuala ya uchaguzi atatakiwa akate rufaa.
a)      Waziri wa Sheria na Katiba atashirikiana na viongozi wa madarasa kupata wajumbe wa Tume ya uchaguzi.
b)      Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi atawasiliana na mwenyekiti wa kamati ya nidhamu ili kuiwezesha Tume hiyo ifanye kazi zake zote kifedha.
c)      Mwenyekiti wa kamati ya nidhamu atahusika katika mchujo wa wagombea ili kujiridhisha na mwenendo mzima wa uchaguzi.
d)     Kiongozi yeyote wa Tume ya uchaguzi ambaye atajihusisha kwenye uchochezi wowote wa kampeni au rushwa atavuliwa madaraka mara moja na kamati ya nidhamu itakaa mara moja ili kuchagua mwingine.
e)      Tume ya Uchaguzi ambayo itajitegemea yenyewe itajumuisha wanachuo   wawili kutoka kila darasa na itashughulikia mambo yote yahusuyo Uchaguzi na taratibu za Uchaguzi.

 12.2 Wanachuo wanaostahili kugombea nafasi ya Rais na Makamu Rais wa ARITASO.

i) Mtu yeyote aliyesajiliwa kuwa mwanachuo wa Chuo cha Ardhi Tabora anaruhusiwa   
kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya Aritaso.Pamoja na hilo atatakiwa kutimiza   
vigezo vifuatavyo:
a) Mwanachuo yeyote anayetarajia kugombea Uongozi katika Serikali ya Wanachuo     haruhusiwi kuwa mjumbe wa Tume ya Uchaguzi.
b) Mwanachama yeyote wa ARITASO ataruhusiwa kuchaguliwa kuwa Rais wa ARITASO ikiwa ana muda usiopungua mwaka mmoja ndani ya ARITASO.
c) Asiwe kiongozi wa chama chochote cha siasa Tanzania.
d) Endapo hajatimiza vigezo na masharti ya kuwa mwanachama wa ARITASO kama    
   ilivyo tamkwa na katiba hii hataruhusiwa kugombea nafasi hizo za uongozi.
e) Asiwe ana historia ya kufanya makosa ya jinai na kuhukumiwa jela kwa makosa hayo

f) Asiwe na histora ya kufukuzwa au kusimamishwa masomo kwa tuhuma ya utovu   
         mkubwa wa nidhamu  kama vile kujihusisha na ngono, ubakaji, vurugu dhidi ya   
         Wanachuo wenzake au wafanyakazi wa Chuo, wizi,  Ulevi, uuaji n.k

ii) Chaguzi zingine zote tofauti na Uchaguzi Mkuu wa ARITASO na uchaguzi wa Spika na    
    Naibu Spika na Katibu wa Baraza la wawakilishi zinatakiwa kufanyika   wiki   
    moja kabla ya uchaguzi mkuu na zifanyike kwa mujibu wa taratibu na kanuni za uchaguzi    
    za ARITASO zitakazo wekwa na Baraza la Wawalikishi.

iii) Viongozi wote wa ARITASO (yaani Baraza la Uendeshaji, Baraza la Wawakilishi na     
Kamati ya Nidhamu) waliopo madarakani kabla ya kufanyika chaguzi zilizotajwa na katiba hii wataendelea kubaki madarakani hadi siku ya kuapishwa kwa viongozi wapya. Kwa kiongozi yeyote atakaye taka kugombea nafasi yoyote ya uongozi atakuwa moja kwa moja amejiondoa kwenye nafasi yake aliyokuwa nayo kabla hajaamua kugombea nafasi anayoitaka. Kwa hiyo atahesabiwa kama mwana- ARITASO wa kawaida na si kama kiongozi tena na nafasi yake atateuliwa mtu mwingine kuishikilia kwa muda kama kuna ulazima wa kufanya hivyo kama hakuna ulazima itabaki wazi hadi pale kiongozi mpya  atakapo teuliwa/kuchaguliwa.

iv) Kiongozi yeyote aliyepo madarakani haruhusiwi kwa namna yoyote ile kuingilia masuala   
ya uchaguzi isipokuwa kamati ya nidhamu pekee au kama kuna jambo la lazima itabidi awasiliane na Tume ya Uchaguzi.

12.3 Wagombea wa Urais na Makamu wa Rais wa ARITASO

a)      Wanachuo wote wanaotaka kugombea nafasi ya Urais au Makamu wa Rais watachunguzwa na Tume ya Uchaguzi baada ya kujaza fomu za maombi.
b)      Mgombea yeyote atalipia fomu kiasi cha Tsh.10000/= kwenye kamati ya nidhamu na kupewa stakabaadhi ambayo itamuwezesha kwenda kuchukua fomu ya kugombea kwenye tume ya uchaguzi.
c)      Muda wa kuchukua na kurudisha fomu hizo utatangazwa na Tume ya Uchaguzi kwa wanachuo wote. Mgombea atakayejaza fomu hiyo kabla au baada ya muda uliotangazwa na tume hiyo fomu yake haitajadiliwa na kwa hiyo jina lake litaondolewa mara moja.
d)     Kama idadi ya wagombea waliochukua fomu ni zaidi ya wagombea watatu kwenye   
     kila nafasi ya uongozi, mchujo utafanyika hadi yabaki majina matatu kwa kila nafasi ya   
     uongozi. Mchujo huo utafanywa na Tume ya Uchaguzi baada ya kuwahoji wagombea   
     kila mmoja peke yake.
Majina matatu ya wagombea kwa kila nafasi kati ya nafasi hizo mbili yatafikishwa   
      kwenye Mkutano Mkuu wa Wanachuo ili yapigiwe kura.
e)      Mgombea atakuwa mshindi kama atapata zaidi ya nusu ya kura zote zitakazopigwa.
      Kama idadi ya wagombea waliochukua fomu za uongozi kwenye nafasi zilizopo ni   
      chini ya wagombea watatu kwenye kila nafasi ya uongozi, basi majina yaliyopo ndiyo   
      yatakayofikishwa kwenye mkutano mkuu wa wanachuo ili kupigiwa kura. Sio lazima    
      yawepo majina matatu.
f)       Tume ya Uchaguzi inatakiwa kutangaza majina ya wagombea waliopitishwa na Tume   hiyo kwa ajili ya kupigiwa kura, ndani ya masaa ishirini na manne baada ya kuwahoji  wagombea hao.
g)      Mgombea ambaye jina lake litaondolewa kwenye kugombea nafasi ya uongozi atapewa    barua inayoeleza kwanini ameondolewa kwenye kinyang’anyiro hicho.

h)      Tume itatakiwa kuendesha chaguzi zote za viongozi wa ARITASO yaani uchaguzi wa   
viongozi wa mabweni, wawakilishi wa madarasa na uchaguzi mkuu ndani ya siku kumi   
toka siku tume hiyo iundwe. Ndani ya siku hizo kumi kutakuwa na siku tatu za kampeni   ambazo zinatakiwa ziwe siku za masomo ili kuruhusu wagombea kunadi sera zao    
Madarasani.Masomo katika siku hizo za kampeni yatasitishwa.

i)        Kutakuwa na karatasi maalum za kupigia kura ambazo zitaandaliwa na tume ya          uchaguzi. Matokeo ya uchaguzi yatajazwa kwenye fomu maalum zitakazokuwa          zimeandaliwa na tume ya uchaguzi na matokeo ya uchaguzi yatabandikwa  kwenye ubao    
wa matangazo.
j)        Endapo mgombea katika nafasi yoyote ya uongozi hajaridhika na matokeo hayo      ataiona tume ili yeye mwenyewe pamoja na tume wazihesabu kura ili aridhike.
k)      Kama mgombea huyo bado hajaridhika na matokeo hayo na ana ushahidi wa kutosha     juu ya ubadhirifu wa kura, atakata rufaa kwenye kamati ya nidhamu ya ARITASO  kwa kuandika barua kwa mwenyekiti wa  kamati hiyo ndani ya masaa  sita baada ya matokeo   kutangazwa. Mwenyekiti ataitisha kikao cha kamati ya nidhamu pamoja na tume ya   uchaguzi ili kulijadili suala hilo. Endapo mgombea atashinda kwa kuonyesha ushahidi   wa  kutosha, mwenyekiti wa kamati ya nidhamu atatangaza kuwa matokeo ya uchaguzi ni batili kwa hiyo uchaguzi utarudiwa ndani ya siku mbili tangu kubatilishwa kwa matokeo   hayo.Hakutakuwa na kampeni tena na uchaguzi utarudiwa kwa nafasi iliyoleta utata tu.  
l)         Watakaobainika kusababisha ubadhilifu wa kura watawajibika kwa kuondolewa kwenye   tume na watu wengine watachukua nafasi zao, wala hawatapewa posho ya wajumbe wa   tume ya uchaguzi.

12.4 Uchaguzi wa Spika, Naibu Spika na Katibu wa Baraza la wawakilishi

i)        Kikao cha kwanza cha Baraza la wawakilishi kitafanyika ndani ya siku sita baada ya uchaguzi mkuu.

ii)      Spika wa Baraza la Wawakilishi atachaguliwa ndani ya siku sita baada ya   uchaguzi mkuu kufanyika

iii)    Endapo kwa sababu yoyote ile uchaguzi wa Spika utashidikana kufanyika ndani ya        siku sita baada ya uchaguzi mkuu, Baraza la wawakilishi linaweza kuongeza muda wa kufanya uchaguzi huo, muda huo wa nyongeza usizidi siku tatu na kikao hicho kiwe ni kwa ajili ya  kumchagua Spika, Naibu Spika na katibu wa Baraza la wawakilishi pekee.

12.5 Malipo ya wajumbe wa Tume ya Uchaguzi

Ili kuondoa wasiwasi Wajumbe wote wa Tume ya Uchaguzi hawatalipwa mshahara   isipokuwa watawezeshwa kifedha ili kufanikisha utendaji kazi wao kama ilivyo tamkwa   katika ibara ya 10.5 (b) ya katiba hii. 

12.6 Mambo mengine yote yahusuyo utaratibu wa chaguzi za Aritaso yatakuwa kama itakavyofafanuliwa katika kanuni na taratibu za chaguzi za ARITASO itakayotungwa na Baraza la wawakilishi.

12.7 Kuapishwa kwa viongozi

Viongozi wafuatayo watatakiwa kula kiapo cha uaminifu kabla hawaanza majukumu yao katika nafasi walizo chaguliwa/kuteuliwa.
a)      Rais wa ARITASO, Makamu wa Rais na Katibu Mkuu wa ARITASO, hawataanza majukumu yao waliyopewa ya uongozi mpaka wale kiapo cha uaminifu kwa mkuu wa Chuo, mbele ya Mshauri wa wanachuo na Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi ya ARITASO.
b)      Spika,Naibu spika na Katibu wa Baraza la wawakilishi hawataanza majukumu yao waliyopewa mpaka wale kiapo cha uaminifu kwa Mkuu wa Chuo, mbele ya mshauri wa wanachuo wa Chuo cha ardhi Tabora na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya ARITASO.
c)      Mawaziri, Manaibu waziri hawataaza majukumu yao ya uongozi waliyopewa mpaka wale kiapo cha uaminifu kwa Mkuu wa Chuo mbele ya Mshauri wa wanachuo wa Chuo cha ardhi Tabora na Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi ya ARITASO.

12.8 Muda wa Kuapishwa.

 Rais wa ARITASO atamtangaza Waziri Mkuu na Baraza la Mawaziri ndani ya siku nne        
 baada ya uchaguzi mkuu kufanyika kwa ajili ya kuthibitishwa na Baraza la wawakilishi.   
 Kwa hiyo viongozi wote wanaotakiwa kula kiapo cha uaminifu wataapishwa ndani ya siku  kumi baada ya uchaguzi mkuu kufanyika.

IBARA YA KUMI NA TATU

MAPATO NA UKAGUZI WA FEDHA ZA ARITASO

13.1 Mapato ya ARITASO yatatokana na:-

a) Miradi mbalimbali ya ARITASO
b) Zawadi
c) Michango kutoka kwa Wanachuo na Wafadhili wowote watakaojitokeza.
13.2 ARITASO itaendesha shughuli yoyote itakayokubalika na mamlaka ya Chuo kwa ajili ya kutafuta fedha kwa ajili ya mfuko wake.
13.3 ARITASO itaweza kuajiri mtu yeyote kuendesha shughuli za kiuchumi kwa niaba yake ikionekana inafaa kwa ushirikiano na mamlaka ya Chuo.
13.4ARITASO inaweza kuidhinisha ukaguzi wa mahesabu (matumizi na mapato) ya fedha kutoka sehemu yoyote ile iwe ndani au nje ya Chuo.
13.5 Fedha ya ARITASO itakaa kwenye account ya ARITASO.
13.6 Fedha ya ARITASO itatumika kwa manufaa ya ARITASO tu kadri yatavyopangiliwa na Baraza la Wawakilishi pamoja na Baraza la Uendeshaji la ARITASO.  
13.7 Waziri wa fedha au Katibu wa Wizara hiyo ndio watakaofuatilia michango kutoka   kwa     
        mhasibu wa Chuo na kuzipeleka Benki
13.8 Wizara ya fedha itabuni miradi ili fungu la Wana ARITASO liongezeke.
13.9 Waziri wa fedha ataandaa taarifa ya fedha ya kila mwezi na ataisambaza kwenye   mihimili yote mitatu ya ARITASO si chini ya mara mbili kila muhula wa masomo.
13.10 Kutakuwa na taarifa ya mkaguzi wa ndani wa mahesabu ya akaunti zote za Chuo cha  Ardhi Tabora kila mwaka .
13.11       Rais wa ARITASO ataidhinisha malipo yote ya ARITASO.
13.12       Waziri wa fedha atamkabidhi waziri mkuu vivuli vya Nyaraka zote za mapato na matumizi ya ARITASO kila baada ya siku kumi na nne. 
13.13 Fedha zote za ARITASO zirejeshwe benki kabla ya kwenda likizo au mafunzo kwa vitendo. Kwa waziri yeyote atakaye ondoka na fedha za ARITASO bila ruhusa ya maandishi kutoka kwa katibu Mkuu wa ARITASO Mwenyekiti wa ARITASO atakuwa na uwezo wa    kumpa barua ya onyo kali na ikiwezekana kuvuliwa madaraka aliyonayo.

IBARA YA KUMI NA NNE

MENGINEYO:

14.1Mambo ya Kuzingtia

   i)        Orodha ya majina na picha za viongozi wa ARITASO itaifadhiwa katika              
         nyaraka za ARITASO
   ii)      Hakuna Mwanachuo au kikundi cha Wanachuo kitakachotumia jina la    
      ARITASO bila idhini ya maandishi ya Katibu Mkuu wa ARITASO.
   iii)    Mshauri wa wanachuo ( Dean of student) ndiye atakayekuwa mshauri mkuu wa serikali yote ya ARITASO na atatakiwa kuhudhuria vikao vyote vya wanachuo wa chuo cha Ardhi Tabora.
   iv)    Kila kiongozi atapewa cheti cha uongozi katika nafasi aliyokuwa nayo.Vyeti  
      hivi vitaadaliwa na uongozi utakaoingia madarakani na ili kiongozi apewe cheti,     lazima atimize kipengele cha (14.1.9) cha katiba hii na lazima aidhinishwe na  Baraza  la uendeshaji la uongozi mpya kwa kushirikiana na mshauri wa  wanachuo
    v)      Mwanachuo wa Chuo cha Ardhi Tabora akifiwa na Baba, Mama, Mke, Mume au Mtoto atapatiwa pole kiasi cha shilingi Elfu 40,000/= kutoka kwenye mfuko wa ARITASO.
   vi)    Mwana ARITASO wa kike akipata mimba aruhusiwe kuahirisha masomo na baadaye kurudia mwaka alioachia kwa ruhusa ya Bodi ya Chuo pasipo kipingamizi chochote.
   vii)   Kutakuwa na Wawakilishi watatu (Waziri wa Elimu, Naibu Waziri wa Elimu na mjumbe mmoja wa Wizara) wa ARITASO kwenye kamati ya mitihani ya Chuo itakayotathimini matokeo ya mitihani ya mwisho wa mwaka.
   viii)   Kutakuwa na Wawakilishi wa ARITASO kwenye kamati ya chakula ya Chuo itakayoshughulikia masuala ya chakula cha Wanachuo itakayoamua hatua ya chakula kisichoridhisha.
   ix)    Kiongozi ambaye hakumaliza muda wake wa uongozi kwa sababu mbalimbali    
      mfano kujiuzuru, kuondolewa kwenye uongozi kwa sababu ya ubadhilifu wa   
      mali ya umma au uzembe au utovu wa nidhamu,hatapewa cheti cha uongozi.
             Ili kiongozi apewe cheti ni lazima awe amekaa madarakani kwa muda       
            usiopungua angalau miezi mitatu.
   x)      Marufuku kwa waziri yeyote kwenda likizo na nyaraka za  
           ARITASO. Kila kiongozi azirejeshe nyaraka za sekta yake kwenye ofisi ya  
           ARITASO kabla ya kuondoka kwenda likizo.
x i)    ARITASO kwa kushirikiana na mshauri wa wanachuo itatakiwa kuandaa ripoti  ya kila mwisho wa mwaka na kuipeleka kwenye uongozi wa chuo.
x ii)  Kiongozi yeyote wa ARITASO asiyewajibika kwenye nafasi yake ya uongozi bila taarifa yoyote kwa uongozi wa ARITASO hatahusika katika mchakato wa kuwezeshwa kifedha.

IBARA YA KUMI NA TANO

MAREKEBISHO YA KATIBA

i)        Katiba hii inaweza kufanyiwa marekebisho endapo theruthi mbili ya wajumbe wote wa   Baraza la Wawakilishi watakubali uamuzi huo. Kinachotakiwa Waziri wa sheria na katiba ataandaa muswada wa marekebisho ya katiba kwa kuzingatia sheria na taratibu za chuo.
ii)      Baraza la wawakilishi litaunda kamati maalum ya marekebisho ya katiba ambayo    itakusanya maoni juu ya muswada uliotolewa wa marekebisho ya katiba.
iii)    Kamati ya baraza la wawalikishi ya kushughulikia marekebisho ya katiba,itakusanya     na kuyawasilisha kwenye baraza la wawakilishi maoni na mapendekezo juu ya marekebisho ya katiba hii kwa ajiri ya kutolewa maamuzi.
iv)    Baraza la wawakilishi litayatolea maamuzi maoni na mapendekezo ya marekebisho ya katiba kwa kusahihisha, kupunguza au kuongeza maoni au mapendekezo mengine kadri litakavyoona inafaa.
v)      Ili kurekebisha katiba hii baraza la wawakilishi litaitisha kikao maalum kwa ajili ya marekebisho ya katiba na theluthi mbili ya wajumbe wote wa baraza la wawakilishi wanatikiwa kuhudhuria.ili kupitisha maamuzi ya kurekebisha katiba hii theruthi mbili ya wajumbe waliohudhuria kikao hicho wanatakiwa kukubali uamuzi huo.
vi)    Rasimu ya katiba itaandaliwa na kuwasilishwa kwa wanachuo ili kutolewa maoni ikikubaliwa inatangazwa rasmi na mkuu wa chuo kuwa katiba ya ARITASO.